Home Uncategorized TANZANIA PRISONS, KAGERA SUGAR WAIGOMBANIA SAINI YA NYOTA HUYU SIMBA

TANZANIA PRISONS, KAGERA SUGAR WAIGOMBANIA SAINI YA NYOTA HUYU SIMBA


MOHAMED Rashid ‘Mo Rashid’ anayekipiga Simba kwa sasa ameziingiza vitani timu nyingi za Ligi Kuu Bara zinazohitaji saini yake ikiwa ni pamoja na Kagera Sugar na Tanzania Prisons.


Mo Rashid amemaliza mkataba wake ndani ya KMC ambapo alikuwa anacheza kwa mkopo.

Habari zinaeleza kuwa Simba imeonyesha nia ya kumpeleka kwa mkopo kukipiga JKT Tanzania msimu ujao.

Mo Rashid amesema kuwa kazi yake ni mpira hivyo bado anafikira ni dili ipi itakuwa ya maana ili akakipige msimu ujao.

“Kazi yangu ni mpira hivyo sina hiyana kwenye timu ambayo itahitaji saini yangu kikubwa ni makubaliano na viongozi wangu wa Simba,” amesema.
SOMA NA HII  KIONGOZI SIMBA ALIPATA TABU SANA NA BAO LA MORRISON ALILITAZAMA KWENYE WHATSAPP