Home Uncategorized MBWANA SAMATTA APANIA KUTUPIA MABAO MENGINE MENGI ZAIDI UBELGIJ

MBWANA SAMATTA APANIA KUTUPIA MABAO MENGINE MENGI ZAIDI UBELGIJ


MTANZANIA,Mbwana Samatta anayekipiga kwenye timu ya KRC Genk sasa anazidi kuifukuzia rekodi yake ya mabao 23 aliyoifunga msimu uliopita.

Samatta kwa sasa amefikisha jumla ya mabao manne ndani ya kikosi hicho kinachotetea taji lake la ubingwa nchini Ubelgiji.
 Hat trick aliyoipiga kwenye mchezo wa jana dhidi ya Waasland na kikosi hicho kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 katika mechi ya Ligi Kuu Ubelgiji imemuongezea kasi Samatta.
 
Licha ya Genk ndio waliokuwa ugenini hakukumuzia Samatta ambaye ni nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘TiafaStars’ kucheka na nyavu na alifunga mabao hayo katika dakika za 52, 66 85. Huku Joseph Paintsil akitangulia kufunga la Kwanza katika dakika ya 21.


Samatta amesema kuwa : “Ni jambo la furaha kwa timu yangu kushinda na kuibuka na ushindi, mwanzo mzuri kwa ajili ya baadaye nia ninatarajia kupiga nyingine zaidi,”.

SOMA NA HII  KUBWA KULIKO KUTIKISA JUMAMOSI DAR, RATIBA KAMILI HII HAPA – VIDEO