Home Uncategorized MBASHA AANIKA HISIA ZAKE LIVE KWA FAIZA ALLY BAADA YA KULIA KISA...

MBASHA AANIKA HISIA ZAKE LIVE KWA FAIZA ALLY BAADA YA KULIA KISA SUGU, AMTAKA AENDE KWAKE


“Mwanamke mrembo sana huyu lakini kavimba macho kwa ajili ya kumlilia mwanaume asiyemtaka. 

“Dah! Faiza kwanini ung’ang’anie mtu asiyekutaka wakati sisi tunaokupenda tupo hapa? Yaani unavyolia unaniliza na mimi maana kwa jinsi ninavyokupenda sitaki kabisa kukuona ukiwa unalia.



“Faiza ulisema haunitaki kwa kuwa mimi sina sura mbaya, lakini kumbuka kuwa watu wenye sura mbaya unaowataka huwa wanakuwa na roho mbaya kama sura zao, maskini binti wa kigogo, machinga wa ki sure kumbuka kuwa mimi niko single na ninakupenda sana, isitoshe na mimi najua maumivu ya mapenzi hivyo ukija kwangu hautajuta kabisa maana nitakulinda kama mboni ya jicho.

“Faiza baby, wahenga hawakuwa wajinga pale waliposema, mpende akupendaye, asiyekupenda achana naye.. Usiruhusu moyo wako kuwa na matobo kama tenga kwa ajili ya kung’ang’ania usipotakiwa, njoo kwangu mama nikuonyeshe upendo, isitoshe mimi nimeokoka na ni mcha Mungu hivyo naijua thamani ya mwanamke kwenye maisha yangu.

“Una watoto wawili na mimi ninae njoo tulee watoto mama, njoo nikuonjeshe raha ya kuvaa shela na pia kuvaa pete ya ndoa. My dear Faiza nakosa cha kusema ila naomba ukitua tu bongo kutokea China unitafute, nimeuandaa moyo wangu kukupokea kama malkia waaa……….. I love you so much.. Mwaaaaaaa….@faizaally_ NATAKA HABARI NJEMA SITAKI HABARI MBAYA.

SOMA NA HII  ISHU YA LIGI KUSIMAMISHWA SIMBA WAIGUSIA, WAICHOKONOA KIANIA KLABU NYINGINE