Home Uncategorized BAADA YA SAMATTA KUTUAA ENGLAND, MTANZANIA MWINGINE ATUA UFARANSA

BAADA YA SAMATTA KUTUAA ENGLAND, MTANZANIA MWINGINE ATUA UFARANSA


Kinda wa Azam FC U-20 na Ngorongoro Heroes, Tepsi Evance Theonasy kutoka Cambiasso Sports amewasili Ufaransa katika Club ya FC Nantes kwa ajili ya kukuzwa kisoka hadi atakapotimiza miaka 18 mwaka huu na kusaini rasmi na timu ya wakubwa FC Nantes.

FC Nantes ni miongoni mwa club zinazoshiriki Ligi kuu nchini Ufaransa, wenzake Tepsi waliochaguliwa bado hawajapata visa ya kwenda kuungana na timu katika nchi za Cech Repunlic au Sweden.

Tepsi aliibuliwa katika clinic ya Cambiasso Sports na Rainbow Sports mwisho wa mwezi wa Novemba 2019 Uwanja wa Uhuru chini ya scout mashughuli kutoka Rainbow Sports Alex Morfaw.
SOMA NA HII  MABAO YA KASEKE YAACHA REKODI TAIFA