Home Uncategorized YANGA YAWASHUKURU MASHABIKI YAWAITA NAMFUA JUMATANO

YANGA YAWASHUKURU MASHABIKI YAWAITA NAMFUA JUMATANO


JUMA Abdul, nahodha msaidizi wa Yanga kuwa watapambana kwenye mechi zao zilizobaki kutokana na kutokuwa na matokeo mazuri kwenye mechi zao mbili za hivi karibuni.

Yanga ilipoteza mbele ya Kagera Sugar kwa kufungwa mabao 3-0 ikapoteza pia mbele ya Azam FC kwa kufungwa bao 1-0 mchezo wake unaofuata ni dhidi ya Singida United utakaochezwa Jumatano, Januari, 22 Uwanja wa Namfua.

Abdul amesema:” Ahsanteni mashabiki wetu kwa kuja na tunawaomba tusikate tamaa tumepoteza mchezo wa pili mapambano bado yanaendelea tutafanyia kazi makosa yetu,”.

Yanga ipo nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 25 baada ya kucheza mechi 14 itamenyana na Singida United iliyo nafasi ya 19 na pointi 10.

SOMA NA HII  MANULA AZIKUMBUKA KELELE ZA MASHABIKI BONGO, ALIA NA CORONA