Home Uncategorized BREAKING: YANGA KUMENOGA, YAMSHUSHA GWIJI ALIYEKUWA BENFICA

BREAKING: YANGA KUMENOGA, YAMSHUSHA GWIJI ALIYEKUWA BENFICA


YANGA leo imemshusha Bongo, Carraca Antonio Domingoz Pinto ambaye alikuwa Mtendaji Mkuu (General Manager) wa Klabu ya Benfica ya Ureno kwa muongo mmoja (miaka 10) ili kuanza kazi ya kushauri kueleka Mabadiliko ya kimfumo ya uendeshaji wa Klabu.

Nguli huyo wa mfumo wa Soka la Kisasa ameletwa kwa hisani kubwa ya Gsm ambao ni wadhamini wa Yanga.

Leo amepokelewa na Makamu Mwenyekiti wa Yanga Fredrick Mwakalebela na Mkurugenzi wa Uwekezaji wa GSM Mhandisi, Hersi Said, Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere terminal 3.

SOMA NA HII  WAMBURA AVIFUNGIA VIWANJA VITATU LIGI KUU