Home Uncategorized HESABU ZA MTIBWA SUGAR ZIPO NAMNA HII

HESABU ZA MTIBWA SUGAR ZIPO NAMNA HII


ZUBER Katwila, Kocha Mkuu wa Mtibwa Sugar amesema kuwa bado wanapambana kurejesha makali ya kikosi chake katika Ligi Kuu Bara.

Mtibwa Sugar imekuwa na mwendo wa kusuasua kwenye mechi za hivi karibuni ambapo ndani ya mwezi Februari kwenye mechi 8 ilizocheza zenye pointi 24 iliambulia pointi 4 kwa kushinda mechi moja mbele ya Ndanda FC kwa mabao 2-0 na sare moja mbele ya Tanzania Prisons huku ikiyeyusha pointi 18 jumla.

Katwila amesema : “Ushindi unatafutwa siku zote na mahitaji yetu ni kuona tunarejea kwenye ubora wetu, bado nafasi ya kufanya vizuri ipo na tunaendelea kujipanga ili kurejea kwenye ubora wetu,”.

Mtibwa Sugar ipo nafasi ya 14 imecheza mechi 26 kibindoni ina pointi 28.

SOMA NA HII  ALIYEMTUNGUA MANULA NDANI YA MBAO ANA JAMBO LAKE JINGINE TENA