Home Uncategorized NAHODHA NAMUNGO ATAJA KINACHOMPA HALI YA KUJIAMINI AKIWA UWANJANI

NAHODHA NAMUNGO ATAJA KINACHOMPA HALI YA KUJIAMINI AKIWA UWANJANI

NAHODHA wa timu ya Namungo, Relliats Lusajo amesema kuwa anatumia muda mwingi kujifunza kwa wachezaji wa kigeni na ndani jambo linalompa hali ya kujiamini.

Akizungumza na Saleh Jembe, Lusajo amesema kuwa amekuwa akitumia muda mwingi kujifunza kutoka kwa wale waliofanikiwa pamoja na nyota wa nje ya Bongo ili kuwa makini.

“Mchezo wa mpira ni kujifunza kila siku kwa kuwa vitu vipya vinakuja na mambo mapya yanakuwa mengi kila siku.

“Kikubwa ambacho ninakifanya nikiwa nyumbani hata mazoezini napenda kuwatazama wenzangu wanafanya nini ili nami nifanye pia,”.

SOMA NA HII  AZAM FC YAPANIA KUFANYA MAKUBWA MBELE YA WAZIMBABWE