Home Uncategorized NAHODHA WA MBWANA SAMATTA AOMBA RADHI

NAHODHA WA MBWANA SAMATTA AOMBA RADHI


JACK Grealish, nahodha wa Aston Villa ameomba radhi baada ya kuvunja agizo la Serikali la kujifungia ndani wakati huu wa mlipuko wa virusi vya Corona.

Grealish, anacheza na nyota wa Tanzania Mbwana Samatta, amesema rafiki yake ndiye amemshawishi kufanya kosa hilo.


“Kila mtu kujifungia ndani ni wakati mgumu kwa sasa, nilipata simu kutoka kwa rafiki yangu akitaka nikamuone kwake, na kwa ujinga, nilikubali kufanya hivyo. Sitaki mtu yeyote afanye kosa kama hili, hakika nahitaji kukaa nyumbani na kufuata maagizo yaliyowekwa” amesema.

Ligi Kuu England imesimamishwa kwa sasa kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona inatarajiwa kurejea Aprili 30 iwapo hali itakuwa njema.

SOMA NA HII  NDANDA YATOSHANA NGUVU NA SIMBA NANGWANDA