Home Uncategorized GUARDIOLA ANAREJEA BARCELONA

GUARDIOLA ANAREJEA BARCELONA

WINGA wa zamani wa Barcelona,  Trevor Sinclair amesema kuwa huenda kocha huyo akarejea ndani ya klabu hiyo.

Guardiola yupo zake ndani ya Manchester City na aliinoa Barcelona 2008 mpaka 2012 na aliweza kutwaa mataji kadhaa ikiwa ni pamoja na lile la Ligi ya Mabingwa Ulaya. 

Mkataba wake na City unatarajiwa kumeguka mwaka 2021 inaelezwa kuwa anataka kusepa.

Winga huyo amesema ishu ya Guardiola kurejea Barcelona ni suala la muda tu kwa sasa. 

“Unapokuwa umeenda mbali halafu moyo wako ukafikiria kurudi utarudi tu, nafikiri mtu anayeweza kumrejesha Guardiola Barcelona ni Joan Laporta (Rais wa zamani wa Barcelona).

SOMA NA HII  MASHABIKI WAITWA UWANJA WA MKAPA KESHO KUISAPOTI STARS SAA 4 USIKU