Home Uncategorized DIDA ANA KAZI NZITO YA KUFANYA NDANI YA LIPULI

DIDA ANA KAZI NZITO YA KUFANYA NDANI YA LIPULI


DEOGRATIUS Munish,’Dida’ maisha yake ndani ya Lipuli yalianza kwa kusuasua ana kazi nzito ya kurekebisha makosa yake wakati Ligi Kuu Bara itakaporejea kuanzia Juni 13.

Alijiunga na Lipuli akiwa ni mchezaji huru kwenye dirisha dogo baada ya kumalizana na Simba.Mechi 8 amefungwa mabao 16 huku Lipuli ikifunga mabao nane.
Mechi zake :-Ruvu Shooting 3-1 Lipuli, Februari 20, Yanga 2-1 Lipuli, Februari 5, Lipuli 1-1 JKT Tanzania Februari 11,Mbeya City 2-1 Lipuli, Februari 18, Tanzania Prisons 2-0 Lipuli, Februari 23, Lipuli 1-2 Namungo , Februari 29, Lipuli 3-3 Ndanda, Machi 3, Machi 10, Lipuli 0-1 Kagera Sugar.

Kocha Mkuu wa Lipuli, Nzeyimana Mailo amesema kuwa kwa sasa anatumia muda mwingi kujenga kikosi imara ambacho kitakuwa na ushindani pale ligi itakapoanza.

“Wachezaji wote nimewapa majukumu ya kufanya ili kuwa bora kwani wengi hawakuwa wakifanya mazoezi wakati ligi iliposimama kutokana na janga la Virusi vya Corona,” amesema.

SOMA NA HII  EXCLUSIVE!! MZEE KILOMONI SI MDHAMINI TENA SIMBA SC, USHAHIDI HUU HAPA