BREAKING: Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba SC, Senzo Mbatha ametangaza kujiuzulu nafasi yake katika klabu hiyo,leo Agosti 9.
Senzo ameishukuru klabu kwa mafanikio yaliyopatikana kwenye kipindi kifupi.
Kwa msimu wa 2019/20, Senzo ameweza kushuhudia timu ikitwaa mataji matatu ambayo ni pamoja na ngao ya jamii, Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho.
Habari zinaeleza kuwa sababu ya kujiweka kando ni kutokuwa na maelewano mazuri ndani ya Simba kwenye masuala ya uongozi.