Home Uncategorized SUAREZ RUKSA KUSEPA BARCELONA, ATLETICO MADRID YATAJWA

SUAREZ RUKSA KUSEPA BARCELONA, ATLETICO MADRID YATAJWA


 LUIS Suarez, mshambuliaji wa Barcelona anatajwa kuingia kwenye anga za Juventus baada ya mabosi wa timu hiyo kukubali kumuacha aondoke ndani ya timu hiyo. 

Atletico Madrid inatajwa kuiwinda saini ya nyota huyo baada ya dili lake la kuibukia Juventus kubuma.


Nyota huyo ametumia miaka sita ndani ya Barcelona ambapo amecheza jumla ya mechi 283 amefunga mabao 198.

Alikuwa miongoni mwa utatu wa MSN akiwa na Messi, yeye mwenyewe Suarez na Neymar ndani ya Barcelona.

Aliibukia Barcelona kwa dau la pauni milioni 74 akitokea Klabu ya Liverpool mwaka 2014 na ameweza kutwaa mataji manne ya La Liga, manne ya Copa de Reys, Championi League na Kombe la dunia la Klabu 2015.

SOMA NA HII  Amunike kujaribu wengine leo