Home kimataifa KANE AGOMEWA KUONDOKA NA KOCHA

KANE AGOMEWA KUONDOKA NA KOCHA


 KOCHA Mkuu wa Tottenham, Nuno Esprito Santo amesema kuwa mshambuliaji wake mahiri, Harry Kane hataondoka kwenye timu hiyo.

Kumekuwa na taarifa kwamba nyota huyo anaweza kusepa na timu ambayo inatajwa kuwa karibu kunasa saini yake ni Manchester City.

Kane ni mfungaji bora katika Ligi Kuu England msimu wa 2020/21 baada ya kutupia mabao 23.

Klabu ya Manchester City inaelezwa kuwa imeweka dau la pauni milioni 150 ili kupata saini ya nyota huyo ambaye inaelezwa kuwa aliomba kuondoka.

Taarifa kutoka kwenye timu hiyo zinaeleza kuwa kocha huyo mpya hataki kuona mchezaji huyo anaondoka na yeye hatakubali kuona akiuzwa. 

SOMA NA HII  RASMI...ZIDANE KUPISHANA NA POCHETTINO PSG....AITWA CHAP QATAR KUMALIZANA NA MATAJIRI...