Home Habari za Simba Leo DABI YA KASI AGOSTI 8…SIMBA NA YANGA KITAELEWEKA

DABI YA KASI AGOSTI 8…SIMBA NA YANGA KITAELEWEKA

habari za SIMBA NA YANGA

Huenda Alhamisi tukashuhudia Dabi yenye kasi zaidi kulingana na namna ambavyo vikosi vya timu zote mbili vimekuwa vikicheza.

Katika mchezo wa kirafiki dhidi ya APR, Fadlu ameonyesha kuwa ni kocha mwenye kupenda soka la kushambulia kwa kasi, kila ambapo wachezaji wake walipokuwa wakivuka nusu ya pili ya uwanja walikuwa wakisuka mashambulizi yao kwa haraka.

Uwepo wa wachezaji wenye kasi katika maeneo yake ya kati (kiungo) na pembeni kama vile, Joshua Mutale, Mzamiru Yassin, Jean Charles Ahoua, Edwin Balua, Ladack Chasambi, Débora Fernandes Mavambo na Awesu Awesu uliwafanya kufika kwa haraka kwa wapinzani wao.

Simba ina mabadiliko makubwa ya kiuchezaji hata wakati ikiwa haina mpira wamekuwa wepesi wa kuutafuta. Mabadiliko hayo ya kiuchezaji na kwa namna ambavyo Yanga nao wamekuwa na kasi kuanzia nyuma hadi eneo lake la mwisho la ushambuliaji ni wazi kwamba itakuwa mechi kali na yenye mvuto wa aina yake.

TATIZO SIMBA

Miongoni mwa mambo ambayo yanampasua kichwa Fadlu ni pamoja na eneo lake la mwisho la ushumbuliaji na hilo limejidhihirisha katika michezo minne waliyocheza ya kirafiki.

Unaweza kuona katika mabao tisa waliyofunga Simba ni bao moja tu lililofungwa na mshambuliaji wa kati kiasili ambaye ni Steven Mukwala, wakati wakiwa Misri kwa maandalizi ya msimu ujao Fadlu alikiri kuwa na kazi ya kufanya juu ya eneo hilo.

Kuwa na wachezaji wa maeneo mengine wenye uwezo wa kufunga ni faida lakini kocha huyo kutoka Afrika Kusini anataka kuona washambuliaji wake wakiwa na wastani mzuri wa kutumia nafasi ambazo wamekuwa wakizitengeneza.

Akimzungumzia Mukwala ambaye alikuwa akicheza soka la kulipwa Ghana, kocha wa zamani wa Yanga na Azam FC, Hans van der Pluijm anaamini mshambuliaji huyo anaweza kuwa suluhisho ndani ya kikosi cha Simba.

“Nimemwona akicheza hapa Ghana, ni kati ya washambuliaji wazuri sana, unajua wapo wachezaji ambao wanaweza kuanza kuonyesha makali yao kwa haraka na wengine huhitaji muda, anaweza kuchanganya mbele ya safari, ni mshambuliaji mwenye nguvu, kasi na maarifa,” alisema kocha huyo raia wa Uholanzi anayeishi Ghana.

SHIDA KWA YANGA

Bado Yanga imeonekana kuwa na shida katika ishu ya kuzuia mipira ya juu, mfano mzuri ni bao walilofungwa na Ricky Banda katika kilele cha Wiki ya Mwananchi.

Banda alifunga kwa kichwa akiruka peke yake mbele ya Aziz Andabwile ambaye katika mchezo huo alitumika kama beki wa kati ndani ya dakika 45 za kipindi cha kwanza huku akicheza sambamba na Dickson Job.

Akizungumzia hilo, kocha wa timu za vijana wa Azam FC, Mohammed Badru alisema: “Hili ni tatizo kwa timu nyingi za Tanzania, mwalimu (Gamondi) anatakiwa kulifanyia kazi.”

SOMA NA HII  JANGA LA KITAIFA...WALINDA MILANGO WAZAWA