Home Uncategorized UFAFANUZI NAMNA KAGERA ILIVYOSHUKA DARAJA

UFAFANUZI NAMNA KAGERA ILIVYOSHUKA DARAJA


Kwa mujibu wa takwimu kutoka Bodi ya Ligi kabla ya michezo GD ya Stand United ilikuwa -9 na GD ya Kagera Sugar ilikuwa -11 matokeo ya Leo

FT’ JKT Tanzania 2-0 Stand United 
FT’ Mbao FC 1-1 Kagera Sugar

Maana yake Stand United imebaki na pointi zake 44 na GD ya -11 na Kagera Sugar imekuwa na Pointi 44 na GD ya -11

Kwa maana hiyo GD zinafanana wote -11 kinachofuata ni Head to Head mechi ya kwanza ya Stand na Kagera ilifanyika Shinyanga na Matokeo yalikuwa 1-1 na mechi ya pili ilifanyika Kagera matokeo Stand ilishinda kwa magoli 3-1

Maana yake Stand anakuwa na Faida kwenye Head to Head. Na kwa mjibu wa takwimu hizo African Lyon na Kagera Sugar wameshuka moja kwa moja na Stand United na Mwadui FC zinacheza Play Off.

SOMA NA HII  SIMBA YAFUNGUKIA ISHU YA MADAWA KWENYE VYUMBA PAMOJA NA AC