PATRICK Aussems, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa kutokana na ratiba ya michuano ya Ligi ya Mabingwa kutoka ni lazima afanye mabdiliko kwenye ratiba zake za maandalizi.
Ratiba ya michuano ya kimataifa ya awali inaonyesha kuwa Simba itacheza mchezo wake wa awali kati ya Agosti 9/10/11 na timu ya UD DO Songo ya Msumbiji.
“Mchezo huu ni muhimu sana tunatakiwa kubadili kidogo programu yetu sababu tunatakiwa kuwa tayari kwa hiyo michezo miwili.
“Hatukutarajia haya kala hivyo imekuwa mshangao kwetu hatukutarajia iwe hivi ila hamna namna, tunahitaji kubadili ratiba yetu ili kuwa tayari kwa michuano mikubwa,” amesema.
Simba imeweka kambi nchni Afrika Kusini kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya unaotarajiwa kuanza Agosti 23.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.