Home Uncategorized LEO SAMATTA KUKIWASHA TENA, USO KWA USO NA MSHIKAJI WAKE GUARDIOLA

LEO SAMATTA KUKIWASHA TENA, USO KWA USO NA MSHIKAJI WAKE GUARDIOLA

LEO Mbwana Samatta, mshambuliaji anayekipiga timu ya Aston Villa atakuwa na kazi ya kukipiga mbele ya Manchester City kwenye mchezo wa Kombe la Carabao.

Mchezo huo utapigwa Uwanja wa Wembeley na unatarajiwa kuwa na upinzani mkubwa kutokana na asili ya fainali za kuwa ngumu kwa timu zote.

Samatta ataweka rekodi ya kukutana uso kwa uso na mastaa wa Manchester City ambao ni akina Aguero,Kocha Mkuu Pep Guardiola.

Villa ilitinga hatua ya fainali kwa ushindi wa mabao 3-2 baada ya mchezo wa kwanza kutoshana nguvu na Leicester kwa kufungana bao 1-1 na kwenye mchezo wa pili wa nusu fainali, Villa ilishinda mabao 2-1 na ulikuwa mchezo wa kwanza kwa Samatta.

SOMA NA HII  KISA SIMBA, KOCHA YANGA AKIWASHA TENA, AWATAJA TFF