Home Uncategorized SIMBA YATOA TAMKO KUHUSU PENALTI MBILI ZA KAGERE

SIMBA YATOA TAMKO KUHUSU PENALTI MBILI ZA KAGERE


HASSAN Dilunga, kiungo mshambuliaji wa Simba amesema kuwa kukosa kwa penalti kwa mshambuliaji wa Simba Meddie Kagere ni sehemu ya mchezo ana imani atajifunza na kurejea kwenye ubora wake.

Kagere mwenye mabao 14 kwenye Ligi Kuu Bara, ndani ya mwezi Februari amekosa penalti mbili ambazo zilipanguliwa na makipa alianza mbele ya Biashara United kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara wakati Simba ikishinda mabao 3-1 na mchezo wa pili ulikuwa wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Stand United wakati Smba ikitinga hatua ya robo fainali kwa ushindi wa penalti 3-2 penalti yake ilipanguliwa.

“Kila kitu kina sababu hivyo kwa Kagere kukosa penalti sio jambo la ajabu, penalti hazina mwenyewe ila kwa kuwa amekosa atajifunza na atarejea kwenye ubora wake,” amesema.

SOMA NA HII  YANGA:NDEMLA AONDOKE SIMBA KUTAFUTA CHANGAMOTO MPYA