Home Uncategorized SIMBA YATOA TAMKO KUHUSU ISHU YA TSHISHIMBI

SIMBA YATOA TAMKO KUHUSU ISHU YA TSHISHIMBI

BAADA ya nahodha wa Yanga, Papy Tshishimbi kusema kuwa hajaongeza kandarasi ndani ya klabu yake hiyo uongozi wa Simba umesema kuwa unatamani siku moja acheze ndani ya Simba.

Tshishimbi amekuwa kwenye ubora wake ndani ya Yanga ambapo ikiwa imefunga mabao 31 amehusika kutoa pasi moja ya bao wakati Yanga ikishinda bao 1-0 mbele ya Biashara United Uwanja wa Taifa.

Nahodha huyo amesema kuwa hana tatizo kuhusu kucheza ila kikubwa anachokitazama ni maslahi.

Kupitia ukurasa wake wa Istagram, Ofisa Hatari wa Simba, Haji Manara amesema:-“Box 2 Box Midfielder Papy Tshishimbi siyo siri mimi nnamshabikia kinoma.

“Nikiulizwa atamani siku moja aje kucheza Simba, Yes (ndio) napenda iwe hivyo ila kwa sasa bado,…But u never know (huwezi kujua) ya kesho.

SOMA NA HII  AZAM, SIMBA NA YANGA ZAKUTANA KWA MFUMANIA NYAVU NAMBA MOJA LIPULI