Home Uncategorized WATATU KIKOSI CHA KWANZA WA YANGA LEO KUIKOSA JKT TANZANIA

WATATU KIKOSI CHA KWANZA WA YANGA LEO KUIKOSA JKT TANZANIA


LEO, Juni 17 Yanga itakuwa kazini ikimenyana na Klabu ya JKT Tanzania Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Itakosa huduma ya wachezaji wake watatu ambao ni chaguo la kwanza la Kocha Mkuu, Luc Eymael kutokana na sababu mbalimbali.

Papy Tshishimbi, nahodha wa Yanga bado hajawa  fiti kutokana na kusumbuliwa na majeraha, Lamine Moro beki tegemezi anasumbuliwa na maumivu ya mguu aliyapata kwenye mchezo dhidi ya Mwadui FC.

Kuanza kwake leo itategemea na maamuzi ya Eymael kwa kuwa amekuwa ni mhimili kwenye safu ya ulinzi.

Kiungo mshambuliaji, Bernard Morrison bado hajajiunga na timu kwa kuwa bado yupo Dar hajaibuka Dodoma kwa kile alicheleza kuwa bado ana maumivu ya goti.

SOMA NA HII  KISA KICHAPO MBELE YA SIMBA, KOCHA AWACHANA WACHEZAJI WAKE JUU YA KIWANGO