Home Habari za michezo AHMED ALLY : KWA HALI HII INABIDI TUVUKE MAKUNDI KWA NAMNA YEYOTE

AHMED ALLY : KWA HALI HII INABIDI TUVUKE MAKUNDI KWA NAMNA YEYOTE

Habari za Simba leo

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema kwa levo waliyofikia itakuwa ni aibu kwao kutofuzu hatua ya makundi hivyo, watafanya kila linalowezekana kuhakikisha wanashinda.

Ahmed ameyasema hayo leo Septemba 27, 2023 alipokuwa akiuzungumzia mchezo wao wa Jumapili Oktoba 1, 2023 dhidi ya Power Dynamos utakaotoa hatma yao ya kwenda hatua ya Makundi.

“Huu mchezo CAF wanauangalia, wanaangalia timu ya CAF Football League. Itakuwa ni aibu eti timu ya CAF Football League halafu isiwepo hatua ya makundi,” alisema Ahmed.

SOMA NA HII  SIMBA KUMEKUCHWA...MAKOCHA WAWILI KUTUA...STRAIKA LA MABAO KUTOKA GHANA LATAJWA...